Mwanamuziki Rashid Makwilo Child Benz "CHUMA" imezidi kuwa mbaya baada ya kutoroka kwenye Nyumba ya Matibabu Sober House alipokuwa akipatiwa matibabu kutokana na kuathiriwa na Matumizi ya Dawa za Kulevya.
Kwa kadri Picha zake zinavyosambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii inayoonyesha dhahiri kuwa Mwanamuziki huyo hali yake inazidi kuwa mbaya tofauti na alivyotoka kwenye nyumba ya Matibabu ambapo aliweza kurekodi Wimbo na Pia kutumbuiza katika Matamasha kadhaa ya Muziki.
Tayari Babu Tale aliyekuwa amejitolea kumsaidia awali alisema hawezi kumsaidia tena kwani alishafanya hivyo ikashindikana na kusema Chid Benz ni sawa na Sikio la kufa halisikii Dawa.
Licha ya kuwa inadaiwa kuwa hataki kupatiwa matibabu lakini dhahiri kuwa kwa hali yake ilivyo sasa anahitaji msaada tena wa Haraka zaidi kuweza kuyanusuru Maisha yake. Hizi hapa Picha za Mwanamuziki huyo kwa sasa :