Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi mkuu wa TFF Revocatus Kuuli amemtangaza Wallace Karia kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kufuatia uchaguzi wa shirikisho hilo uliofanyika leo Makao Makuu ya Tanzania Dodoma.
Wallace Karia ameibuka mshindi wa nafasi ya Urais wa shirikisho hilo huku nafasi ya Makamu ya Rais ikichukuliwa na Michael Wambura, kwa matokeo hayo Wallice Karia anakuwa mrithi wa aliyekuwa Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Jamal Malinzi Katika uchaguzi huo wajumbe waliweza kuchagua Kamati ya Utendaji wa TFF katika kanda mbalimbali ambao ni
Sarah Chau (Arusha na Manyara)
Mbasha Matutu (Shinyanga & Simiyu
Vedastus Lufano (Mara na Mwanza)
Mohamed Abeid (Dodoma & Singida)
Dustan Ditopile (Lindi & Mtwara)
James Patrick (Njombe & Ruvuma)
Lameck Nyangaya (DSM)
Khalid Mohamed (Kilimanjaro na Tanga)
Francis Ndulane (Pwani na Moro)
Elias Mwanjala (Mbeya & Iringa)
Kenneth Pesambili (Rukwa & Katavi)
Issa Mrisho (Kigoma & Tabora)
Salum Chama ( Kagera na Geita)

Rais wa TFF Wallace karia akifurahi jambo Mara baada ya kutangazwa Rais wa TFF.