Nahodha wa timu ya Taifa stars Mbwana Samatta ametupia magoli 2 kwenye mchezo dhidi ya Botswana katika dk 2 na 88.
Mbwana Samatta ametimiza ahadi yake kwa Watanzania ambayo aliahidi kabla ya mchezo mapema juzi alivyokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
Katika Mchezo huo uliofanyika uwanja wa taifa waziri mpya wa Habari Sanaa na Utamaduni Harson Mwakyembe alihudhuria kwenye mchezo huo akiwa na aliyekuwa waziri wa Wizara hiyo Nape Nnauye.