SAFARI YA ROMELU LUKAKU YAIVA KUTUA MIKONONI MWA MOURINHO. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

SAFARI YA ROMELU LUKAKU YAIVA KUTUA MIKONONI MWA MOURINHO.

Manchester United wameafikiana na klabu ya Everton kulipa £75m kumchukua mshambuliaji Romelu Lukaku ambapo usiku wa Alhamisi hii anadaiwa kupelekwa Los Angeles Marekani, kwaajili ya kufanyiwa vipimo ili kukamilisha deal hilo.

Mazungumzo kuhusu kuhama kwa Lukaku hayahusiani na mazungumzo kuhusu uwezekano wa mshambuliaji wa United Wayne Rooney kurejea Everton. Klabu hiyo ya Jose Mourinho ina matumaini kwamba itakamilisha usajili wa Lukaku kwa wakati kumuwezesha kujiunga na kikosi cha timu hiyo kitakachosafiri kucheza mechi za kabla ya msimu nchini Marekani Jumapili.

Mshambuliaji huyo alikuwa miongoni mwa orodha ya wachezaji ambao Mourinho aliwasilisha kwa naibu mwenyekiti wa klabu hiyo Ed Woodward kwamba alitaka kuwanunua kabla ya msimu kumalizika.

Awali, ilidhaniwa Lukaku angerejea katika kalbu yake ya awali Chelsea, ambayo alijiunga nayo kutoka Anderlecht mwaka 2011. Mshambuliaji huyo aliuziwa Everton kwa £28m na Mourinho mkufunzi huyo kutoka Ureno alipokuwa katika kipindi chake cha ukufunzi Chelsea mwaka 2014.

Lukaku ni mteja wa wakala Mino Raiola, ambaye pia huwasimamia Paul Pogba, Zlatan Ibrahimovic na Henrikh Mkhitaryan – wachezaji watatu walionunuliwa na United majira ya joto msimu uliopita.

Mbelgiji huyo alikataa ofa ya juu sana kutoka Everton Machi na kusema: “Sitaki kusalia katika kiwango sawa. Ninataka kujiboresha na najua ni wapi nahitaji kwenda out in is a hilo.”

Romelu lukaku

SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More