Tino Ze Mastermind: May 2017

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

NEDDY : DOGO JANJA HANA ADABU.

Msanii Nedy Muziki anayefanya poa na ngoma yake "Doze"amejibu kauli ya Dogo Janja anayexema hajui kuvaa amesema Dogo huyo hana Adabu kwa watu wazima ndio maana ametoa kauli hiyo kwake ambaye ni  kaka yake kwenye mitupio.
    Nedy ametoa jibu hilo kwenye kipindi cha 5Selekt cha EATV kwa kusema kwamba Dogo janja kumfananisha na Mkongo kwenye suala la kuvaa ni kukosa adabu ndio maana hata alipojua amekosea akaanza kujitetea kwamba watu wanawapambanisha.
"Dogo Janja hana heshima ndiyo maana aliweza kuzungumza kauli ile, Naweza kumfananisha na kijana anayeweza kuwakuta wazee wamekaa bila kusalimia alafu akauliza mbona hamjanisalimia wakati ni wajibu wake kuanza kuwasalimia . Sasa Janjaro ni mdogo wangu kwenye suala la mavazi. Mtu ambaye anawaza kukaa chini na kunipambanisha naye atakuwa ana matatizo ya akili na achunguzwe vizuri" - Neddy Music.
Pamoja na hayo Neddy ameweka wazi kwamba hana Matatizo yoyote na msanii huyo ambaye kwa sasa anasumbua masikio ya mashabiki zake inayokwenda kwa jina la 'Ukivaaje unapendeza' ndiyo maana hakutaka kubishana naye au kutengeneza bifu.

IGP SIRRO Atangaza Dau nono kwa atakayetoa Taarifa ya Mauaji Kibiti.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro, avalia njuga matukio ya uhalifu yanayoweka rehani amani ya nchini.
Awali IGP Sirro ametuma Salamu za kwa wahalifu na kuwapa neno la faraja Wananchi wa Kibiti , Ikwiriri pamoja na Mkuranga na Rufiji.
IGP Sirro amekula kipao mbele ya suala la Mauji ya Raia kibiti na kuweka Dau kwa Wananchi watakao waonyesha wauaji wa Raia.
Ameweka mikakati ya kutokomeza uhalifu huo kwa kuanza kuongeza nguvu ya ziada kukabiriana na uhalifu huo.
Suala la Pili la ni Rushwa kwa Askari wa Jeshi la Polisi na kwamba askari au mtumishi wa jeshi hilo akicjihusisha na Rushwa atachukuliwa hatua za kisheria.
Suala la Mwisho ni kwamba kukomesha mauji yanayotokana na wananchi kujichukulia sheria Mkononi (watu wenye asira kali) na kwamba watachukuliwa hatua Kali.

MAZISHI YA IVAN : WATOTO WA MAREHEMU WATOA UJUMBE WA MWISHO MATAJIRI WAMWAGA PESA KWENYE KABURI.

Shughuli ya kuuzika mwili wa mfanyabiashara maarufu nchini Uganda na Afrika Kusini ambaye pia alikuwa mume wa Zarina Hassan, Ivan Ssemwaga zinaendelea katika makaburi ya ukoo wake yaliyoko Kayunga, nchini Uganda.
Zari akiwa na watoto wake mbele ya jeneza

Baada ya jana Zari kutoka kauli yake ya kwanza toka Ivan kufariki, Leo watoto wa marehemu wametoa kauli yao ya mwisho kwa marehemu baba yao.

Soma taarifa hii…

“Dad, so many thoughts come to our mind whenever we speak of your name; it seems without you in our lives things will never be the same. We think of the good old days when we were still so little; consumed in your love, and in your smile.”

“Those days are gone and no matter what we do, life will never be the same! Oh Dad, if only we could turn back the hands of time and hear your voice once more, but God called you to a better place, so peaceful and free of pain. And when we see you sleeping, we can only wish the best for you.”


Ivan Semwanga alifariki katika Hospitali ya Biko Academy nchini Afrika Kusini, Alhamisi wiki iliyopita kutokana na ugonjwa wa moyo na anazikwa leo.

IVAN KUZIKWA LEO : ZARI AAHIDI KUWAANGALIA WATOTO

Baada ya Jumatatu hii mwili wa Ivan Ssemwanga kuagwa na kufanyiwa ibada takatifu, aliyekuwa mke wa zamani wa marehemu, Zari Hassan alipata fursa ya kuzungumza kwa mara ya kwanza. Katika misa ya mazishi iliyofanyika kwenye kanisa la Namirembe mijini Kampala, Uganda Jumatatu hii, Zari alionekana akiwa ametulia na akizungumza na wanae. Alipoitwa kuzungumza madhabahuni, watu waliohudhuria walijianda kumsikiliza atakachosema. “Sitomhuzunikia Ivan,” alisema. “Nitasherehekea maisha yake. Muda mrefu, tulitengana kwasababu ya tofauti ambazo sote tulizijua. Nilisonga mbele na maisha yangu, lakini si Ivan. Ivan alijua kile nilichoweza kufanya. Alijua kile nilichoweza kufanya na kile nisichoweza. Alijua kuwa ningewaangalia vijana vyema na aliniamini. Kwa hali hiyo, naahidi ntawaangalia vijana hadi nitakapoungana naye.” Ivan anatarajiwa kuzikwa leo ambapo Diamond aliyezaa na Zari watoto wawili naye aliahidi atahudhuria.
Zari akiwa na watoto wake kwenye misa hiyo

TANZIA : MZEE ALIYECHORA NEMBO YA TAIFA AFARIKI.

Mzee Francis Kanyasu aliyechora Nembo ya Taifa amefariki dunia usiku wa kuamkia leo akiwa kwenye matibabu Hospital ya Muhimbili.
Taarifa iliyotolewa na Hospital hiyo iliandika.

HABARI KATIKA PICHA:

TANZIA : Meya wa Mji mdogo wa Urambo, Ndg. Peter Sitta amefariki dunia katika Hospitali ya Hindu Mandali alikokuwa amelazwa akitibiwa. Ndg. Peter Sitta ni Mdogo wa Marehemu Mh.Samweli Sitta msiba upo nyumbani kwa Hayati Samweli Sitta mtaa wa Twiga karibu na makao makuu ya UNHCR.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY 28 2017.

Kurasa za Magazeti ya Leo Jumapili May 28 kuanzia vichwa vya Habari vya Siasa Jamii Dini na Michezo nimekusogezea hapa.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MAY 25 2017.

Nimekusogezea kurasa za Magazeti ya Leo Alhamisi 25 2017 kuanzia kurasa za Magazeti kuanzia vichwa vya Habari vya Siasa Jamii na Michezo.