Majeruhi wa ajali ya Basi la wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent waliopelekwa nchini Marekani imeripotiwa hali zao kuendelea vizuri huku mmoja kati yao Wilson kwa Mara ya Kwanza ametoka nje.

Taarifa iliyotolewa na Mbunge wa Singida Kaskazini Mh Lazaro Nyalandu imeeleza kuwa mtoto Doreen amemaliza kufanyiwa upasuaji wa Uti wa Mgongo kwa kile ambacho Madaktari wamesema wamefanikiwa kwa Ufanisi Mkubwa kupita matarajio yao.
Doreen alikuwa afanyiwe upasuaji kwa makadirio ya Masaa 5.30 lakini zoezi hili lilikamilika kwa mda wa Masaa 4 huku timu ya "Surgical "ikiwa na watu sita na kwa Pamoja wakiongozwa na Madaktari Bingwa wawili Dr. Meyer na Dr. Durward.
Doreen amehamishwa katika chumba cha Upasuaji na kupelekwa ICU ambako wamempumzisha baada ya upasuaji na kumrudisha wodi ya watoto ambako ataendelea na mapumziko.Mungu amesikia maombi ya Watanzania na wote waliotoa Sala zao kwa ajili ya mtoto Doreen popote Duniani.