Ajinyonga Hadi Kufa Baada Ya Mkewe Kumnyima Samaki. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Ajinyonga Hadi Kufa Baada Ya Mkewe Kumnyima Samaki.

Mkazi mmoja wa kijiji cha Kalunde kilichopo Kata ya Kipande wilayani Nkasi Vedasti Kazumba 51 amejiua kwa kujinyonga kwa kile kinachodaiwa kuwa alighadhabika baada ya Mkewe kumnyima kitoweo cha Samaki.




Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa George Kyando alithibitisha tukio hilo na kusema lilitokea usiku wa mkesha wa mwaka mpya na kwamba Kazumba alifikia uamuzi huo mgumu kwa kujinyonga akitumia kamba ya Katani.
Alieleza hakuna mtu anayeshikiliwa na Polisi kuhusu tukio hilo na Uchunguzi wake unaendelea.

Habari kutoka kijijini humo kinaeleza kuwa chanzo cha Kazumba kujinyonga ni kukasirishwa na kitendo cha mkewe Antoniata Mwisua kumnyima kitoweo cha Samaki.

"Mke wa marehemu aitwae Antoniata alimwandalia mumewe huyo chakula cha Usiku kitoweo chake kikiwa ni Samaki mbichi Alimkomba samaki huyo kisha akamwomba amwongezee kitoweo kingine cha Samaki,lakini mkewe alimweleza kitoweo kimekwisha ndipo mumewe alipokasirika akidai kuwa
Mkewe amemnyima kwa makusudi kitoweo hicho ndipo alipochukua hatua ya kuzira kula" alieleza mmoja wa mashuhuda kwa masharti ya kutotajwa.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kalunde John Kalasa alidai kuwa marehemu wakati wa Uhai wake alikuwa ni mtu mwenye kujawa na Ghadhabu ambapo Mara kadhaa alisikika akitishia kujinyonga.
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More