Klabu ya Tottenham imefutilia mbali ndoto ya Chelsea kutaka kuweka historia katika ligi kuu ya England kushinda michezo 14 baada ya vinara hao kufungwa bao 2_0 ndani ya Uwanja wa White Hart Lane.
Spurs wamesogea mpaka nafasi ya 3 ya msimamo wa ligi baada ya mchezaji wake Dele Alli kufunga magoli yote mawili kwa njia ya kichwa ikiwa ni mwishoni mwa kipindi cha kwanza na dakika 54.Dele Alli alifunga vyema kwa kupokea Pasi safi kutoka kwa Christian Eriksen kwa magoli yote mawili.
Eden hazard alikosa nafasi 2 za kuiokoa Chelsea lakini Spurs waliweza kufanikiwa na kuweza kupata Pointi 3 muhimu na kuwaondoa majirani zao Arsenal katika nafasi ya nne.