Mkazi wa Bukene wilayani Nzega mkoani Tabora amemuua mkewe pamoja na mtoto wake.Mkazi huyo Rashid Nassoro baada ya kuwaua watu wake hao wa karibu alikimbia na baadaye kujiua kwa kujichoma kisu tumboni na kujaribu kukata sehemu zake za siri.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora Khamis Selemani amethibitisha tukio hilo na kusema lilitokea juzi eneo la Bukeni wilayani hapa baada ya Rashid Nassoro 22 kumuua mkewe kwa kumchoma visu tumboni.Alisema "baada ya kumuua mke wake Rashid alimnyonga mtoto wake wa miezi minne na kukimbia".
Kamanda Selemani alisema "baada ya kukimbia Rashid aliamua kujiua na kukata sehemu zake za siri".Kamanda Selemani alisema chanzo cha tukio hilo ni mwanamke kumtuhumu mume wake kuwa ana uhusiano na mwanamke mwingine jambo lililomchukiza mwanaume huyo na kuamua kuchukua maamuzi hayo.