Waziri Nchemba Amtembelea Mama Chid Benz na Kufanya naye Mazungumzo. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Waziri Nchemba Amtembelea Mama Chid Benz na Kufanya naye Mazungumzo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba weekend hii alimtembelea mama yake Chid Benz na kufanya Mazungumzo ili kuangalia namna ya kumsaidia Rapa huyo pamoja na kuongeza kasi ya kupambana na Magenge ya wauzaji wa Madawa ya Kulevya.


Hatua hiyo imekuja baada ya wiki iliyopita katika mitandao ya kijamii kuzagaa Picha za Rapa Chid Benz "CHUMA" akiwa katika hali mbaya iliyosababishwa na matumizi ya madawa ya kulevya.Baada ya kufanya mazungumzo na mama Chid Benz kupitia mtandao wake wa Instagram Waziri Mwigulu aliandika:

"Nimekutana na kufanya mazungumzo na mama wa msanii Rashid Makwilo Child Benz ambaye kwa sasa amepatwa na tatizo la dawa za kulevya inasikitisha na haivumiliki kuona nguvu kazi ya Taifa inapotea huku wauzaji wakinufaika kwa Pesa haramu.Ifahamike wazi vita ya Serikali dhidi ya Magenge, Wauzaji na wasambazaji wa madawa ya kulevya imeongezeka hasa katika awamu hii ya 5
Chini ya Mh Rais J.P Magufuli.Hivyo anayejihusisha kwa namna yoyote ni vema akaamua kuachana naye kabla hajakutwa na mkono wa dola.Mbali na vyanzo vya taarifa tulivyonavyo ni wajibu
wa kila aliye RAIA MWEMA kutoa taarifa zitakazosaidia kuangamiza biashara haramu ya madawa ya kulevya. Naishukuru familia ya Chid Benz kwa jitihada wanazofanya kuhakikisha kijana mwenzetu anarejea katika hali yake ya kawaida.Unaweza kuimba, unaweza kufanikiwa, unaweza kutatua matatizo yako bila kutumia madawa ya kulevya"alimalizia waziri Mwigulu.

Hali ya Msanii Chid Benz imeendelea kuwa mbaya baada ya kuzagaa taarifa na picha zikimuonesha akiendelea kutumia dawa za kulevya.
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More