ASLAY NDIYO CHANZO CHA YAMOTO BAND KUVUNJIKA. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

ASLAY NDIYO CHANZO CHA YAMOTO BAND KUVUNJIKA.

Baada ya watu wengi kujiuliza kwa muda mrefu kipi hasa kimepelekea kundi la Yamoto Band kusambaratika licha ya kuwa walikuwa wakifanya vizuri kwenye muziki, msanii mmoja aliyekuwa anaunda kundi hilo amefunguka na kueleza kuwa Aslay ndiye alikuwa chanzo cha wao kusambaratika.

Beka Flavour kutoka Yamoto Band amesema kuwa kundi hilo lilianza kuwa na mgogoro baada ya Aslay kutoa wimbo wa Kidawa bila kumshirikisha mtu yeyote, au hata viongozi wa kundi hilo.
Alipoulizwa sababu za kuchukua uamuzi huo, Aslay anadaiwa alisema kuwa alikuwa akijaribu tu ambapo wimbo huo kwa kiasi fulani ulipokelewa vizuri.

Beka Flavour ameyasema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio na kutanabaisha kuwa baada ya wao kuona Aslay ametoa wimbo wake mwenyewe na wao waliomba uongozi kutoa nyimbo zao wenyewe. Alisema waliona bora na wao watoe nyimbo zao wenyewe sababu kama wangesubiri wangonekana labda hawawezi kuimba wenyewe.
Tayari wasanii wa kundi hilo wameanza kufanya kazi mmoja mmoja huku Aslay akiwa ametoa nyimbo 4 hadi sasa.

Aslay 
Beka Flavour
Yamoto Band zamani kabla ya kuvunjika kwao 
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More