NATAKA KUONDOKA REAL MADRID : CHRISTIAN RONALDO | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

NATAKA KUONDOKA REAL MADRID : CHRISTIAN RONALDO

Baada kuipa mafanikio makubwa klabu yake ya Real Madrid ya Spain, Cristiano Ronaldo ameutaarifu uongozi wa klabu hiyo kuwa anataka kuondoka. Gazeti la A Bola la Ureno limeripoti na kuzihusisha klabu za PSG na Manchester United kuwa ni timu ambazo huenda akajiunga nazo.

Hatua hii ya Ronaldo ambaye pia ni mshindi mara nne wa tuzo ya 'Ballon d'or' inakuja baada ya kupata kesi ya ukwepaji kodi. Katika hatua nyingine gazeti la Marca limeripoti tetesi kuwa Real Madrid imeiambia Man United iandae Pauni 160 milioni, kama inamtaka mkali huyo.

Cristiano Ronaldo licha ya kutetewa na club yake ya Real Madrid kuhusiana na tuhuma za ukwepaji kodi zinazomkabili, ameripotiwa kufikiria kufanya maamuzi magumu.

Cristiano Ronaldo ambaye ni mchezaji tegemeo katika kikosi cha Real Madrid anatuhumiwa kukwepa kodi nchini
Hispania katika kipindi kati ya 2011 hadi 2014 kiasi kinachotajwa kufikia pound milioni 13 ambazo ni zaidi ya Bilioni 35 za kitanzania.

Mtandao wa Sky Sports umeripoti kuwa staa huyo aliyeisaidia Real Madrid kutwaa mataji matatu ya UEFA Champions League anataka kuondoka yeye mwenyewe
Hispania kutokana na tuhuma zinazoendelea ambazo anaamini hafanyiwi haki.

SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More