Mahakama Kuu ya Uganda imeiagiza Benki Kuu ya Uganda kwa kushirikiana na kampuni ya kuandaa mazishi ya A Plus Funeral Management Company Limited iliyonadaa mazishi ya Ivan Semwanga kulifukua kaburi hilo ili fedha zilizowekwa ndani ya kaburi ziweze kutolewa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mahakama hiyo leo Juni 2, fedha zote ambazo ni pamoja na Shilingi ya Uganda, Rand ya Afrika Kusini na Dola ya Marekani na fedha za nchi nyingine yeyote, zitolewa katika kaburi la marehemu Ivan Semwanga aliyezikwa Jumanne Mei 30, 2017.
Aidha, mahakama hiyo imeamuru kuwa mlalamikaji Mgugu Abey aruhusiwe kuzichukua fedha hizo kwa niaba ya Jamhuri ya Uganda na nchini nyingine ambazo fedha zake zilifukiwa.
Hapa chini ni taarifa kutoka kwenye mahakama hiyo;