Msanii wa muziki Diamond Platnumz amekanusha taarifa ambazo zimekuwa zikizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa Hamisa Mobeto ana mimba yake. Aidha muimbaji huyo amekanusha pia kuwahi kutoka kimapenzi na video queen huyo ambaye anatikisa katika tasnia ya urembo.
Akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds Fm Jumatano hii wakati akiutambulisha wimbo wake mpya ‘I Miss You’, Diamond amedai tetesi za yeye kutoka kimapenzi na Hamisa zilianza baada ya kufanya naye kazi katika project ya wimbo, Salome.
“Toka nimeshoot na Hamisa Mobeto wimbo wa Salome, watu wamekua wakituhusisha pamoja, ujauzito wa Hamisa sio wangu,” alisema Diamond. “Jamani mwenye mimba si ajitokeze, si unajua hata mtu wake atakuwa anajisikia vibaya,” Pia muimbaji huyo amedai wasichana wengi ambao anafanya nao kazi upakaziwa kuwa anatoka nao kimapenzi.
"Picha za Zari akiwa kwenye bwawa la kuogelea niliziona mtandaoni, nikapanic sana nikadhani kwamba Mama watoto wangu kazingua, lakini baadae nilifahamu kwamba hakukuwa na tatizo katika picha, kwani yule jamaa ni shemeji yake na hawakufanya lolote baya