Nahodha wa wa timu ya taifa ya Ureno na mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid Christian Ronaldo ameeleza majonzi yake kufuatia msiba uliokumba ulimwengu wa soka baada ya Wachezaji na Viongozi wa klabu ya Chapecoense ya Nchini Brazil kufariki kutokana na Ajali ya Ndege.
Kiasi cha fedha alichochangia Ronaldo kwa klabu ya Brazil iliyopata Ajali ya Ndege.
Ali kiba asherekea siku yake ya kuzaliwa Mbugani,Jokate atuma ujumbe mzito kwake.
Mkali wa Bongo flava Ali kiba jumanne hii aliungana na uongozi wake na familia yake kwenda mbuga za wanyama za Serengeti National Park mkoani Mara kwa ajili ya kusherekea siku yake muhimu katika maisha yhuku
Picha ya Diamond akiwa amevaa Kiboxer yasababisha povu zito Instagram.
Mwanamuziki Diamond Platnumz amejikuta akitupiwa lawama baada ya kupiga picha akiwa amevaa kiboxer.Diamond ambaye ni bingwa wa kusababisha povu kwenye mitandao ya kijamii.Kwenye picha hiyo aliyoweka Instagram Diamond aliandika "Straight from changing room.....I think I need to go back to the gym so that i can be more flexible on m 24th Pre_Xmass Performance in Dar es salaam" alimalizia Diamond.
POLISI YAZUNGUMZIA SAKATA LA ASKARI ALIYEJIUA KWA BAHATI MBAYA.
Jeshi la polisi mkoani Pwani limezungumzia kifo cha askari wake PC Armand Furaha 33 aliyejipiga risasi kifuani bila kukusudia na kufariki dunia.Askari huyo alijipiga risasi hiyo usiku akiwa anaelekea kwenye lindo nyumbani kwa mkuu wa Wilaya ya Kibaha.Tukio hilo lilitokea saa 1 usiku eneo la Maili moja wakati askari huyo akiwa njiani
kuelekea kwenye kituo cha lindo alichopangiwa.
Kaimu kamanda wa polisi Pwani Blasius Chatanda amesema askari huyo alijipiga risasi kwa bahati mbaya kwa bunduki aina ya SMG akiwa amekaa kwenye kiti cha mbele katika gari alilokuwa anasafiria kwenda lindoni.Amesema uchunguzi wa awali umebaini "kuwa askari huyo alikuwa tayari ameweka risasi chemba kwenye bunduki hiyo aliyokuwa nayo na kwa bahati mbaya akiwa anashuka kwenye hilo gari ndipo risasi hiyo ikafyatuka na kumpiga kifuani eneo la kushoto na kufa wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Tumbi".
Kabla ya tukio hilo askari huyo aliwasili kazini jioni na kukuta amepangiwa kituo cha ulinzi cha Mkuu wa Wilaya hivyo kama ilivyo ada alichukua zana za kazi ikiwemo bunduki hiyo na kuanza safari ya kuelekea lindoni kwake huko kwa DC.
Lakini kwa bahati mbaya hakufika alikufa kwa kujipiga risasi bahati mbaya amesema Chatanda.
Akizungumzia suala la kujipiga risasi msemaji wa jeshi la Polisi,Advera Bulimba amesema kila tukio hutokana na mazingira tofauti.
Wananchi wa Cuba watoa Heshima zao za Mwisho.
Maelfu ya raia wa Cuba wametoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi mwanamapinduzi Fidel Castro aliyeaga dunia siku ya ijumaa akiwa na umri wa miaka 90.Raia wengi wa Cuba walikuwa katika milolongo mirefu ya foleni kabla hata ya Alfajiri ili kuhakikisha wako miongoni mwa watu wa kwanza kutoa heshima zao.Katika uwanja wa Revolution Square katika mji Mkuu Havana sehemu ambayo waombolezaji wameweka picha ya kiongozi huyo akiwa ameshika bunduki.
Ndege iliyobeba Wachezaji wa timu ya soka ya Brazil yaanguka Colombia
Ndege iliyokuwa imewabeba watu 81 wakiwemo wachezaji na maafisa wa moja ya klabu kubwa za soka nchini Brazil imeanguka ikikaribia mji wa Medelin nchini Colombia na kuua watu 76.Polisi wamesema watu 5 walinusurika lakini wengine wote waliangamia.Ndege hiyo ya kukodishwa ilikuwa safarini kutoka Brazil ikipitia Bolivia na ilikuwa imewabeba wachezaji na Maafisa wa timu ya Chapecoense.