Maelfu ya raia wa Cuba wametoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi mwanamapinduzi Fidel Castro aliyeaga dunia siku ya ijumaa akiwa na umri wa miaka 90.Raia wengi wa Cuba walikuwa katika milolongo mirefu ya foleni kabla hata ya Alfajiri ili kuhakikisha wako miongoni mwa watu wa kwanza kutoa heshima zao.Katika uwanja wa Revolution Square katika mji Mkuu Havana sehemu ambayo waombolezaji wameweka picha ya kiongozi huyo akiwa ameshika bunduki.
Ilikuwa siku ya kwanza ya kipindi cha siku 6 za maombolezi rasmi ya kifo cha
Fidel Castro.Siku za maombolezi zitakamilika baada ya majivu ya mwili wake kuzikwa siku ya Jumapili.Majivu ya Fidel Castro yatatazamiwa kuwasilishwa kwa umma katika Uwanja wa Revolution Square lakini yatawekwa katika sehemu tofauti.