Aliyekuwa Mbunge wa Kasulu mjini 2010 mpk 2015 kwa tiketi ya Nccr Mageuzi Moses Machali ambaye alihamia Act Wazalendo ameamua kujiunga rasmi na ccm.
Machali ameamua kufanya hivyo baada ya kueleza kuwa ccm ya Rais Magufuli siyo ile ya 2015.Akiongea zaidi Machali amesema tuachane na siasa nyepesi za kutaka kuona kwamba mazuri ni yale yanayofanywa na wapinzani huku mambo hayohayo yakifanywa na ccm yaonekane hayafai na kutajwa kuwa ya hivyo.
Ccm ya JPM siyo ile ya 2015 kurudi nyuma kidogo hii ni tofauti na ninaiunga mkono.Machali ambaye aligombea Kasulu mjini mwaka 2015 kwa tiketi ya Act Wazalendo na kushindwa katika uchaguzi mkuu uliopita amesema kelele wanazopiga baadhi ya watu kwamba maisha yamekuwa magumu kwa sababu ya Magufuli ni Propaganda tu kwa sababu hakuna uhusiano wa maisha magumu na suala la kudhibiti wapiga dili wa fedha na mali za umma amemalizia Machali.