Ndege iliyokuwa imewabeba watu 81 wakiwemo wachezaji na maafisa wa moja ya klabu kubwa za soka nchini Brazil imeanguka ikikaribia mji wa Medelin nchini Colombia na kuua watu 76.Polisi wamesema watu 5 walinusurika lakini wengine wote waliangamia.Ndege hiyo ya kukodishwa ilikuwa safarini kutoka Brazil ikipitia Bolivia na ilikuwa imewabeba wachezaji na Maafisa wa timu ya Chapecoense.
Klabu hiyo ilikuwa imepangiwa kucheza mechi ya final ya Copa Sudamericana dhidi ya timu ya Atletico Nacional ya mji wa Medellin.Mechi ya awamu ya kwanza ya kombe hilo,la pili kwa umuhimu America Kusini ilikuwa imepangwa kuchezwa jumatano lakini sasa imesitishwa.Timu hiyo inayotoka mji wa
Chapeco kusini mwa Brazil ilipandishwa kucheza ligi ya daraja la kwanza nchini Brazil mwaka 2014 na ilifika fainal ya kombe hill la Sudamericana kwa kuilaza San Lorenzo ya Argentina.Maafisa wa klabu hiyo ya Chapecoense wametoa taarifa wakisema "tunamuomba mungu awe na wachezaji maafisa,wanahabari na wageni wengine na watu ambao waliandamana na timu yetu.