Siku chache baada ya kuripotiwa taarifa za kukamatwa mwanaume mmoja raia wa malawi ambaye anadaiwa kufanya ngono na wanawake 104 hatimaye Hukumu ya Mtuhumiwa bwana Eric Aniva mwenye umri wa miaka 45 raia wa nchi ya Malawi aliyekiri kufanya mapenzi na wanawake 104 bila kuwaaambia ya kwamba yeye ni muathirika wa Ukimwi imetolewa nchini Malawi. Hatimaye amehukumiwa kwenda jela miaka MIWILI. Hukumu hiyo ambayo imewashangaza watu wengi imeonesha kutotenda haki kwa wanawake hao kutokana na uchache wa miaka aliyofungwa mwanaume huyo.Michael Chipeta wakili na mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu nchini Malawi amekosoa hukumu hiyo.
Na kusema kuwa kulikuwa na mapungufu mengi katika mchakato mzima wa kesi na hukumu dhidi ya mwathirika Huyo wa Virusi vya Ukimwi.Tayari mashirika ya kutetea haki za binadamu na asasi za kupambana na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi nchini Malawi zimekosoa Hukumu hiyo.Picha ya Mtuhumiwa mwenyewe bwana ERIC ANIVA.