Afariki baada ya kunywa Pombe kali. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Afariki baada ya kunywa Pombe kali.

Mkazi wa mtaa wa Migombani kati ya Kaloleni Halmashauri ya Mji wa Tunduma wilaya ya Momba mkoani Songwe Edmound Josephat 30 amekutwa akiwa amefariki dunia nyumbani kwake baada ya kudaiwa kunywa Pombe akiwa hajala.
Josephat alifariki baada ya kunywa pombe Kali bila kula.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Mathius Nyanga alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kusema alipata taarifa kutoka kwa wananchi wa kijijini hapo."Nilipata taarifa kutoka kwa wananchi wa mtaa huo ambao baadaye waliuchukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi baadaye waliuchukua mwili huo na kuupeleka hospitali ambako iligundulika marehemu alikuwa amekunywa pombe kali bila kula".

Ingawa haikujulikana ni pombe ya aina gani alisema kamanda Nyange.
Kutokana na tukio hilo kamanda Nyange aliwataka wananchi kuacha tabia ya kunywa pombe kali bila kula kwa kuwa kufanya hivyo wanahatarisha maisha yao.

Pamoja na hayo tunaangalia namna ya kuanza kufanya Operesheni ili kuwabaini wanaokunywa pombe wakati wa kazi na wale wanaokunywa pombe haramu zilizopigwa marufuku alisema kamanda.Pia alisema wataanza kuwabana wanaoingiza pombe kutoka nchini Zambia na Malawi kwa kuwa zimekuwa zikiua watu mara kwa mara.

SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More