Mwanamuziki Dogo Janja kutoka kundi la Tip Top Connect amefiwa na baba yake mzazi mzee Abubakari Chende.Dogo Janja kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika "Pumzika kwa amani baba yangu kipenzi hakika mungu amefanya maamuzi yake siwezi kukufuru zaidi ya kukuombea kwa Allah akupe kauli Thabeet umelala baba yangu sitakuona tena EEH MWENYEZI MUNGU UMPOKEE UMUONDOLEE ADHABU ZA KABURI.Lala baba hakika wote njia yetu ni moja siku moja tutaonana tena baba R.I.P Kamanda ABUBAKARI CHENDE.
Mara nyingi Dogo Janja amekuwa akisikika akieleza jinsi baba yake alivyokuwa akimuunga mkono kwenye kazi yake ya muziki anayoifanya.
BREAKING:BABA MZAZI WA MWANAMUZIKI DOGO JANJA AFARIKI DUNIA.
About Author
ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More