Takribani watu 40 wamefariki nchini Kenya kufuatia Lori la kubebea mafuta kulipuka.Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya limetoa taarifa kuwa gari hilo lilikuwa likielekea nchini Uganda lakini lilionekana kumshinda dereva kabla ya kugonga magari mengine na kulipuka eneo la barabara ya Nairobi Naivasha kaskazini Magharibi mwa mji mkuu Nairobi.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa mlipuko mkubwa uliotoka katika gari hilo ulilipua nagari mengine na baadhi ya watu waliokuwa wamesimama jirani na barabara.
Miongoni mwa magari yaliyoteketea ni pamoja na daladala 3 yaliyokuwa na abiria 14 ambao wote wamefariki.Baadhi
ya vyombo vya habari nchini Kenya vinataja idadi ya waliofariki ni zaidi ya 40
Miili mingi kwenye ajali hiyo imeungua kiasi cha kushindwa kutambulika.Hali za
Waliojeruhiwa zinaelezwa kuwa ni mbaya sababu ajali hiyo imetokea ikiwa Madaktari wanaingia katika Siku ya tatu ya Mgomo wao. Hizi hapa baadhi ya Picha za Moto huo :