Mahakama ya wilaya ya Ilala imemhukumu Shabani Huseni miaka 29 kifungo cha Miaka 30 Jela baada ya kupatikana na Hatia ya kunajisi mtoto wa miaka 9.Akisoma hukumu hiyo Hakimu mkazi Catherine Kihoja alisema Upande wa Mashitaka ulipeleka Mashahidi watano ambao wameweza kuthibitisha mashitaka bila kuacha shaka yoyote.
"Kutokana na Ushahidi uliotolewa Mahakamani hapo umeweza kuthibitisha mashitaka hivyo mshitakiwa ninamtia Hatiani kama alivyoshitakiwa"alisema Hakimu Kioja.Kabla ya kutolewa kwa Adhabu hiyo wakili wa Serikali Neema Moshi aliomba Mahakama kutoa adhabu
Kali kwa Mujibu wa Sharia kwa kuwa Mtoto aliyefanyiwa kitendo hicho Ameathirika Kisaikolojia na kupata Madhara kiafya.
Aidha mshitakiwa aliiomba Mahakama impunguzie Adhabu kwa kile alichodai kwamba hana ndugu Ombi ambalo lilitupiliwa mbali.
Inadaiwa Mshitakiwa alitenda kosa hilo Julai mwaka Jana Eneo la Kipunguni B Moshi bar wilayani Ilala ambapo alimbaka binti wa Miaka 9.