Mwimbaji wa muziki wa Asili Saida Kalori ambaye wimbo wake "Maria Salome" umepata mashavu mawili makubwa mwaka huu kwa wakali wa Bongo flava Diamond na Darasa amezungumzia kitendo cha Darasa kuweka vionjo vya wimbo wake huo mpya bila kuomba ridhaa yake.
Darasa aliachia wimbo ambao sasa "watoto wa mjini" wanauita "Wimbo wa Taifa wa Bongo Flava" alioubatiza jina la MUZIKI ukiwa na vionjo vya "Maria Salome siku chache baada ya Diamond kuachia Salome yenye vionjo hivyo ambavyo yeye aliomba ridhaa kwa Uongozi wa Saida".
Akizungumzia uamuzi huo wa Darasa, Saida Kalori amesema kuwa hana tatizo naye kwa kuwa kufanya hivyo amekuza muziki, lakini alitupa lawama kwa Mtayarishaji wa wimbo huo kutoomba ridhaa ya kutumia vionjo hivyo.
Namnukuu "Siwezi kumfanyia chochote Darasa kwa kuwa hii ni njia ya muziki wetu kukua, unaweza kuonekana una roho mbaya ukikataza watu wasitumie kazi zako ila kufuata taratibu ni vizuri zaidi" alimalizia Saida Kalori.
Hivi karibuni Rapa Darasa alisema kuwa alipanga kumshirikisha Saida Kalori kwenye wimbo huo kuweka vionjo lakini aliahirisha baada ya Diamond kuachia Salome kabla yake.