Rais John Pombe Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 5678 ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi Meja Jeneral Projest Rwegasira wafungwa 1340 wataachiwa huru na 4338 watatumikia kifungo kilichobaki baada ya kupunguziwa moja kwa sita za vifungo vyao.Rais ametoa msamaha huo
Kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya ibara ya 45 (1) d ya katiba.
Rwegasira ameeleza kuwa wafungwa wote wamepunguziwa vifungo vyao zaidi
ya punguzo la kawaida linalotolewa chini
ya kifungo cha 49 (1) cha sheria ya Magereza sura ya 58.Amesema wafungwa waliopewa msamaha huo ni pamoja na Wagonjwa wa Ukimwi, Kifua kikuu na Saratani na ambao wamethibitishwa na jopo la waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa au wa Wilaya.
Hizi hapa picha za sherehe za Maadhimisho hayo Uwanja wa Uhuru: