Mahakama ya Hakimu mkazi Tanga imemtia hatiani na kumuhukumu kwenda Jela miaka 25 au kulipa Faini ya sh bilioni 3.7 Mfanyabiashara Charles Kijangwa kwa kujihusisha na biashara ya Meno ya tembo.Mshitakiwa huyo alikabidhiwa mahakamani hapo baada ya kukamatwa na Askari wa kikosi cha kuzuia Ujangili kanda ya Mashariki na Pwani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wilaya ya Lushoto.
Hakimu mkazi Cresian Kisongo ametoa hukumu hiyo kwa Kijangwa ambayo aliruka dhamana tangu mwaka 2010 takribani miaka 6 sasa.Wakili wa Serikali
Mwandamizi Saraji Iboru alidai mahakamani kuwa mshitakiwa Kijangwa
alikuwa akitafutwa na Serikali kwa muda mrefu tangu mwaka 2010 ambapo aliruka dhamana katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 6 ya mwaka 2007 iliyokuwa ikimkabili yeye pamoja na wenzake Michael Msuya na Nyaisa Makori.
Mshitakiwa Kijangwa alitenda kosa hilo November 2005 na April 2006 kwa kusafirisha Makontena mawili ya Tembo yenye Ujazo wa Tani 5000 yaliyokamatwa katika bandari ya Konshug nchini Taiwan.
Makontena hayo ambayo yalitokea katika bandari ya Tanga yakiwa na Shehena ya Kamba za Katani na Meno ya Tembo ndani yake yalikuwa yanapelekwa Manila nchini Philippine.