Mkuu wa wilaya ya Ubungo Humphrey Polepole ameteuliwa na halmashauri kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kuwa katibu wa Halmashauri kuu Itikadi na Uenezi kuchukua nafasi ya Nape Nnauye.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chama hicho kupitia ukurasa wake wa Twitter zinaeleza kuwa Halmashauri kuu kimemteua Polepole kushika wadhifa huo.Kikao cha Halmashauri kuu ya Taifa
CCM kimefanyika Leo ambapo miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa ni pamoja
na Tathimini ya Uchaguzi mkuu mwaka 2015.