Ucku wa tarehe 10 Jumamosi kulifanyika tuzo za EATV AWARDS kwenye ukumbi wa Mlimani City Dar es salaam ukihusisha tuzo zaidi ya 10 zikitolewa katika vipengele tofauti.
Tuzo hizo zilitolewa kwa Mara ya kwanza tangu zianzishwe kwa wasanii wa Bongo Flava na waigizaji wa Bongo Movie.Mgeni rasmi kwenye tuzo hizo alikuwa waziri wa Habari Mh Nape Nnauye na Host wa tuzo hizo alikuwa mkali wa hizi kazi Salama Jabir kutoka Eatv.
Msanii Ali kiba alichukua tuzo 3 huku mwigizaji wa Bongo movie Salim Ahmed
Maarufu kama Gabo akichukua tuzo 2.
Kivutio kikubwa kwenye tuzo ni kutambulishwa kwa mpenzi mpya wa Mwimbaji Lady Jaydee ambaye alipanda naye kuchukua tuzo ya msanii bora wa kike.Baada ya shukrani kwa mashabiki na kutaka kuondoka lady jaydee alirudi jukwaani na kusema "nilitaka kusahau huyu ni baby wangu"kauli ambayo iliibua shangwe kwa mashabiki. Nimekusogezea hapa majina ya Washindi na Vipengele walivyoshinda :
Msanii bora wa kiume 2016 : Ali kiba
Video bora ya mwaka 2016 : Aje Ali kiba
Wimbo bora wa mwaka 2016 : Aje
Mwanamuziki bora chipukizi 2016 : Man Fongo
Filamu bora ya mwaka 2016 : Safari ya Gwalu
Mwigizaji bora wa kiume 2016 : Salim Ahmed Gabo zigamba
Tuzo bora ya Heshima : Dj bonny luv
Mwigizaji bora wa kike 2016 : Chuchu Hans
Kundi Bora la mwaka 2016 : Navy Kenzo
Mwanamuziki bora wa kike 2016 : Lady Jaydee