Msichana Anusurika Kifo baada ya Kujirusha toka Ghorofa Ya Saba Dar es salaam. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Msichana Anusurika Kifo baada ya Kujirusha toka Ghorofa Ya Saba Dar es salaam.

Msichana Redna Raphael mwenye umri wa miaka 19 amenusurika kifo baada ya kujirusha kutoka Ghorofa ya Saba katika Jengo la Harbour View Tower maarufu kama J.M Mail lililopo katika makutano ya mtaa wa Samora na barabara ya Morogoro jijini Dar es salaam.


Redna ambaye ni Mfanyakazi wa kampuni ya Usangu Logistics ltd yenye ofisi zake ndani ya jengo hilo inadaiwa "alichukua uamuzi huo muda mfupi baada ya kuzungumza na simu na mtu ambaye bado hajafahamika wanahusiana vipi".

Hata hivyo binti huyo alinusurika baada ya kuangukia kwenye moja ya Mabomba
yanayotoa moshi kwenye Jenereta ya Jengo hilo lillilopo Ghorofa ya kwanza ambako walinzi wa Jengo hilo walimuokoa.

Meneja wa Kampuni hiyo ya Usangu Mazar Dadkarim alisema wakati tukio hilo linatokea hakuwepo Ofisini bali alipatiwa taarifa na Wafanyakazi wenzake waliokuwa ofisini.
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More