Kocha wa Manchester United Jose Mourinho ametetea uamuzi wake wa kumuingiza uwanjani kiungo wa kati Marouane Fellaini kama nguvu mpya wakati wa mechi ambayo walitoka sare na Everton jumapili katika mechi ya ugenini katika uwanja wa Goodson Park. Zlatan Ibrahimovic aliiwekea Manchester United goli la kuongoza dk 42 lakini Leighton Baines akaisawazishia Everton kwa mkwaju wa Penati.
Fellaini aliingia dk 85 alimfanyia madhambi Idrissa Gueye ndani ya box ambapo Baines hakufanya makosa.
Alipoulizwa kuhusu uamuzi wa kuingiza Fellaini Mourinho alisema "alimwingiza kwa sababu ya kimo chake na uchezaji wa Everton."Nilifikiria kwamba mnafaa kuwa mnajua mengi zaidi kuhusu soka kuliko mlivyo,Everton si timu ya kutoa pasi kama walivyokuwa zamani,Everton ya sasa ni klabu inayocheza moja kwa moja,Ashley William moja kwa moja Ramiro Funel moja kwa moja kila kitu moja kwa moja".
"Anapokuwa na mchezaji wa kimo cha mita mbili kwenye benchi unamchezesha kwenye safu ya ulinzi kuisaidia timu kushinda mipira"alimalizia Jose Mourinho.