.Mshambuliaji wa timu ya vijana ya Mbao Fc under 20 Ismail Mrisho Khalfan anayevalia jezi nambari 4 amefariki dunia baada ya kuanguka uwanjani Kaitaba wakati wa mtanange wao dhidi ya timu ya vijana ya Mwadui Fc ikiwa ni mechi ya mwisho ya kumaliza duru la kwanza la ligi ya vijana.
Ismail khalfan amefariki mara baada ya kufikishwa Hospital ya serikali ya mjini Bukoba.Ismail Khalfan kabla ya kufikwa na umauti aliweza kuifungia timu yake bao la kwanza na la pili lilifungwa kwa mkwaju wa penati hivyo mtanange kumalizika kwa 2_0
Kabla ya kuanguka Ismail aligongana na beki wa Mwadui Fc na baadaye akiwa peke yake alianguka chini lakini aliinuka halafu
akaanguka tena na kutokana na ukosefu wa huduma ya kwanza na gari la wagonjwa katika uwanja wa Kaitaba kulipelekea marehemu kupandishwa gari la zimamoto na kupelekwa Hospital ambapo mauti yalimkuta mchezaji huyo.