Mwanamuziki Darasa na wenzake wamenusurika kifo baada ya kupata Ajali mbaya Kahama akiwa na wenzake wakiwa njiani wakirejea Dar es salaam Maeneo ya Ntobo barabara ya kuelekea Mgodi wa Bullyanhulu wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.
Habari zimeeleza kuwa ndani ya Gari hilo
aina ya Toyota Harrier yenye namba za Usajili T 503 DGQ ambalo dereva hakufahamika mapema Darassa alikuwa
ameambatana na Director Hanscana na Producer Abba Process na wote wametoka salama.
Kupitia Ukurasa wake wa Instagram Darassa amethibitisha kupata ajali hiyo na kama aonekanavyo kwenye Video Clip ya tukio la Ajali hiyo akimshukuru Mungu kwa kutoka Salama yeye Pamoja na wenzake.Nimekusogezea baadhi ya Picha za Ajali hiyo :