Mwanamitindo aliyepata jina mwaka huu kutokana na Uhusiano wa muda Mfupi na Wema Sepetu, Calisah amemwelezea Muigizaji na Miss huyo wa zamani kuwa ni Msichana mzuri na mwenye mapenzi ya Kweli.
"Wema Sepetu ni msichana mzuri, ana upendo ni mwelewa, ana mapenzi ya kweli sijaona kasoro kubwa ambayo anayo tofauti na Wasichana wengine amesema Calisah".
Pia ana msichana anayejua kucare ana real love pia ana mapungufu yake lakini mazuri ni mengi amesisitiza Calisah.
Model huyo ameongeza kuwa kwa sasa yeye na Wema hawazungumzi tena baada ya wiki kadhaa zilizopita kusambaa mtandaoni Video inayowaonesha wakibusiana kwa mahaba mazito.
Kitu ambacho kilimkera Wema Sepetu na kuvunja Uhusiano wao.Hata hivyo Calisah amekiri kuwa Uhusiano wake na Wema umemuongezea Umaarufu zaidi na kumrahisishia kazi zake.