Sababu zinazosadikika kuwa Chanzo cha Vifo vya watu waliokutwa wamekufa Mto Ruvu. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Sababu zinazosadikika kuwa Chanzo cha Vifo vya watu waliokutwa wamekufa Mto Ruvu.

Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba amesema kuwa huenda watu waliokutwa wamekufa na kutupwa kwenye Mto Ruvu kwa kufungwa kwenye viroba walikuwa ni wahamiaji haramu ambao walikumbwa na mkasa huo toka kwa wasafirishaji wa Wahamiaji hao.

Akizungumzia tukio hilo mkoani Singida waziri Mwigulu amesema kitendo cha kukutwa kwa wahamiaji zaidi ya 80 wakiwa na majeraha na hawajiwezi mkoani Pwani kinahusisha kwa namna moja au nyingine maiti zilizookotwa Mto Ruvu.

Waziri Mwigulu amesema kuwa watu hao ambao wamezikwa na Serikali licha ya ndugu au Taifa lolote kujitokeza Sheria inawaruhusu kufanya hivyo kutokana na kutokutambulika kwa watu hao.

Waziri Mwigulu amesema bado wanaendelea na Uchunguzi juu ya Matukio hayo ikiwa na Operesheni mbalimbali za kutokomeza Matukio ya Kihalifu pamoja na Wahamiaji haramu Nchini.
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More