Mkali wa bongo Flava Tunda Man amefunguka sababu inayomfanya asielewane na Bosi wake wa Tip Top Connection Babu Tale.Muimbaji huyo wa "Mama Kijacho" amesema "najuta kuwa na misunderstanding na bosi wangu, Kiukweli mimi na bosi wangu hatuko sawa kosa silijui".
"Kuna kitu mimi nimemkosea may be au ameamua tu kukasirika na kiukweli hii kuwa mbali na Bosi wangu kwenye kazi zangu ninazofanya nakuwa mwenyewe tu kiukweli its pain naumia".Lakini sometimes mtu anaweza akawa na mwanae akamwambia nenda katafute maisha kivyako japo baba yake ana kila kitu.
"Kwa hiyo unakuta mtoto anaondoka kutafuta maisha mengine, anabeba zege,
anafanyaje lakini anajutia kuwa mbali na baba take". Lakini Mimi najutia kwa sababu kazi zangu nakuwa na wakati mgumu wa kuzipush na kusupport kazi zangu Alhamdulilah Mungu anasaidia".
Tunda man ameongeza kuwa kuna kipindi alipata dili la kufanya Tangazo lakini kuna mtu alimpandia na nafasi hiyo akapewa Msanii mwingine anayesimamiwa na Babu Tale.