FRANCIS CHEKA ATANGAZA RASMI KUSTAAFU NGUMI. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

FRANCIS CHEKA ATANGAZA RASMI KUSTAAFU NGUMI.

Bingwa wa Dunia wa ngumi za kulipwa mwenye rekodi ya kutopeza kirahisi mechi zake katika Tanzania anayekipiga uzito wa kati Francis Cheka ametangaza rasmi kuachana na Mchezo huo wa ngumi na kujielekeza kwenye Masuala ya kibiashara.


Cheka "NGUMI JIWE" mwana wa Morogoro amesema haya wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro kuhusu taarifa zilizolipotiwa na vyombo mbalimbali vya habari na kuzagaa kwenye Mitandao ya kijamii vikimhusisha na Utapeli wa kukimbia Ulingoni Disemba 25 mwaka huu jijini Dar es salaam.

Alikotakiwa kupigana na Bondia Dula Mbabe ambapo amebainisha kutofika Ulingoni siku hiyo hakukumaanisha kuhofia Pambano hilo bali ni kutokana na Promota wake Kaike Selagi kutomlipa Fedha zake zote kama walivyokubaliana ambapo amedai alipaswa kulipwa Milioni 9 lakini hadi wanamaliza kupima Uzito alikuwa amepewa milioni 3 pekee.

Akizungumzia azma ya kuachana na Ngumi Cheka amesema kwa muda mrefu amekuwa akipigana bila Mafanikio kutokana na Kudhulumiwa na Waandaaji kulipwa Tofauti na Makubaliano sambamba na Misukosuko ya Hapa na Pale anayofanyiwa na Wapinzani wake na kwamba anaamini wapo baadhi ya watu waliolenga kumshusha kwenye Ngumi badala ya Kumtengeneza Bondia mwingine mwenye uwezo wa kumpiga.

Amesema kwamba kwa sasa atajielekeza kufanya biashara zake na kuahidi ushirikiano kwenye Mchezo wa Ngumi ili kukuza na Kuendeleza Mchezo huo.
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More