Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi SUGU amenusurika kwenye ajali.Taarifa zilizoripotiwa na kituo cha Runinga cha ITV leo Disemba 17 zinasema kuwa Mbunge huyo amenusurika katika Ajali ya gari iliyotokea eneo la Iyunga Jijini Mbeya.
Ajali hiyo imetokea baada ya gari lake kufeli Breki na kumgonga Mtoto mwenye umri wa miaka 15 ambaye amefariki dunia wakati akipelekwa Hospitali.
Aidha Taarifa hiyo inaeleza kuwa Askari Polisi 4 wamejeruhiwa baada ya kupata Ajali wakati wakielekea kwenye ajali hiyo aliyopata Mbunge Joseph Mbilinyi SUGU
Gari hilo la Mbunge huyo lilikuwa linaendeshwa na Dereva wake Gabriel Andrew 43 ambaye anashikiliwa na Polisi.