Mwanamke mmoja raia wa Misri anayeaminiwa kuwa na uzito zaidi duniani akiwa na Kilo 500.Eman Ahmed Abd Aty mwenye umri wa miaka 36 atasafirishwa hivi karibuni kwenda India mjini Mumbai kwa ndege ya kukodishwa kufanyiwa upasuaji wa kupunguza uzito wake.
Dk Muffazal Lakdawala anapanga kumfanyia upasuaji.Ubalozi wa India mjini Cairo ulikuwa umemnyima Visa kwa kuwa hakuweza kufika kwenye Ubalozi huo yeye mwenyewe binafsi.
Hata hivyo hali ilibadilika baada ya Daktari kutoka Mji wa Mumbai kuiandikia
Kwa mashauri ya kigeni ya India kupitia Mtandao wa Twitter.
Familia ya bi Abd El Aty inasema hajaondoka nyumbani kwa miaka 25.
Ikiwa madahi kuhusu uzito wake ni ukweli basi atakuwa mtu mzito zaidi duniani aliye hai kwa kuwa Pauline Potterraia ndiyo anashikia rekodi ya Guinness alikuwa na kilo 292 mwaka 2010.