Mtandao wa kuuza nyimbo za muziki Nchini Mkito.com umetoa List ya Nyimbo 5 za wasanii wa muziki nchini ambazo zimepakuliwa zaidi kupitia Mtandao huo ndani ya mwaka 2016.
Kupitia Akaunti ya twitter Mkito wameandika "tunapofunga mwaka hizi ni baadhi ya Ngoma zilizowavutia watu wengi 2016 hebu tutajie zako 5 ulizozikubali zaidi mwaka huu 2016.
Mtandao huo wa Mkito kwa sasa ni mmoja kati ya mitandao mikubwa Nchini Tanzania ambayo inategemewa na Wasanii kwa kuuza Nyimbo zao.