Cheka Adai Hakupigwa India Aelezea Alichofanyiwa na Mwamuzi. | Tino Ze Mastermind

TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS,MUSIC,VIDEO AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Breaking News
Loading...
TANZANIA NEWS,POLITICS NEWS,CELEBRITY GOSSIP,ENTERTAINMENT NEWS AND SPORTS NEWS 24 HOURS.

Cheka Adai Hakupigwa India Aelezea Alichofanyiwa na Mwamuzi.

Bondia Mtanzania Francis Cheka ambaye mwishoni mwa wiki alipoteza Pambano lake Nchini India alipopigana na Raia wa Nchi hiyo Vijender Singh, ameibuka na kusema kuwa Mpinzani wake huyo hakumpiga ila alibebwa na Mwamuzi.



Akiongea kutoka India Cheka amesema katika raundi ya 3 alipata tatizo katika kifaa chake cha kulinda Meno kwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na Kikohozi na wakati anakifanyia Marekebisho ndipo Mwamuzi akatangaza Mshindi bila ya kumuuliza Cheka mwenyewe kama alikuwa anaendelea au la.

"Tatizo nilikuwa nakohoa, nilijiandaa kumpiga yule Vijender"alisema Cheka.
Pia katika mtandao wake wa Instagram bondia huyo aliandika hivi :

"Pale ambapo Matokeo yamepangwa, tunaenda kukamilisha ratiba tu. Refa unaona Mouth Guard imetoka na Unaendelea kuchezesha........WaTanzania nadhani mmeona, tusiwage wanyonge kwao na kwetu pia.....nadhani nimeliwakilisha Taifa vyema, kuitangaza Morogoro,Tanzania, Kiswahili na Kimakonde Pia" alimalizia Bondia huyo.
SHARE HABARI HII NA WENZAKO WAIPATE
KAMA UKIHITAJI KUWEKEWA MUONEKANO MZURI(BLOG DESIGNING) WA BLOG YAKO KAMA HUU WASILIANA NA RUBEN EMMANUEL KWA NAMBA 0716528779/0755542721 KARIBU SANA

google+

linkedin

About Author
  • ASANTE MSOMAJI WETU KWA KUTEMBELEA BLOG HII MAALUMU KWA HABARI MBALIMBALI, USISITE KUWASILIANA NASI KAMA UNA HABARI PICHA VIDEO MAONI NA USHAURI MATANGAZO YA BIASHARA N.K. NAMBA ZETU NI 0714082857Read More