Kama ulikuwa unadhani mwaka 2016 hautakuwa bora kwa upande wa Christian Ronaldo basi mambo yamekuwa tofauti.Leo Jumapili Disemba 18 Real Madrid imecheza dhidi ya Kashma Antlers kwenye bonge moja la Fainal ya Fifa Club World Cup.
Wenyeji Kashima Antlers walikuwa vizuri
tofauti na watu walivyokuwa wanawachukulia poa baada ya kuwabana washindi wa Champion League 2016 hadi dk 90 ubao ulikuwa unasomeka 2_2.Game ikaelekea kwenye dk za nyongeza na hapo ndipo Ronaldo
akaamua Mchezo huo.
Baada ya Filimbi ya Mwisho Madrid akawa mshindi kwa Magoli 4_2.Ronaldo amefunga Hat_trick kwenye Mchezo wa Vilabu bingwa Duniani.Bao la kwanza lilitokana na Mkwaju wa Penati baada akafunga goli baada ya kuvunja Off Side trick ya Kashima na kuweka kambani.
Akamaliza Hat_trick yake dakika ya 104 kwa shuti Kali la karibu.