Karrueche Tran ni mwanamke ambaye Chris Brown hatokuja kumsahau kamwe.Sijui Karrueche alimpa nini lakini tunachofahamu ni kuwa pamoja na kuachana Hitmaker huyo wa "Party" Chris Brown amekuwa akifuatilia kila nyendo za Mrembo huyo ikiwemo kuwamaindi wanaume wanaommendea.
Mrembo huyo ambaye baada ya kuachana na Chris Brown anaonekana kuwa yupo Single amepost Picha kwenye Mtandao wa Instagram na kuweka Caption rahisi "Baby" kwenye Picha hiyo anaonekana amevaa T_shirt Nyeusi yenye picha ya muimbaji wa
UK Sade na pia amevaa nguo ya ndani yenye rangi nyekundu.
Macho ya Breezy yalivutiwa na alichokiona na kujikuta akicomment "Still Want It".
Pamoja na jitihada zote za kutaka kumrudisha Karrueche kwenye himaya yake Chris Brown "BREEZY" amekuwa akiambulia patupu.