December 2 kwa Mara ya 5 mbunge wa Arusha Mjini Chadema Godbless Lema alikosa dhamana katika mahakama kuu kanda ya Arusha na hivyo kulazimishwa kurudi rumande.
Mbunge huyo alikamatwa Nov 3 mwaka huu akiwa katika vikao vya bunge mjini Dodoma akituhumiwa kutenda kosa la Uchochezi dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli.
Lema alidai kuwa yeye ni mwombaji na alipokuwa akiomba Mungu alimuonesha kuwa Rais Magufuli asipojirekebisha atakufa.Wakati Lema akirejeshwa rumande mke wake na watoto wake walikuwa mahakamani hapo.
Akizungumza na waandishi wa habari mtoto wa kwanza wa Mbunge huyo Allbless Lema alisema "Yeye haoni shida baba yake kuendelea kukaa rumande sababu anapigania haki ya familia yake na watanzania wote".Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena February 2 2017.